Messi awaongoza wanasoka 5 duniani wanaolipwa zaidi, Cristiano Ronaldo akishuka hadhi kifedha
-Cristiano Ronaldo ametemwa kutoka kwenye orodha ya wachezaji watano wa soka duniani wanaolipwa pesa nyingi zaidi
-Gwiji wa Barcelona Lionel Messi yuko kwenye nafasi ya kwanza kwa hisani ya mkataba wake wa hivi majuzi
- Aliyekuwa mchezaji wa Manchester United Carlos Tevez yuko kwenye nafasi ya pili
Licha ya kushinda tuzo ya FIFA ya Ballo d’Or, mshambuli wa Ureno na Real Madrid Cristiano Ronaldo ametemwa kwenye orodha ya wachezaji watano wa soka duniani wanaolipwa pesa nyingi zaidi.
Huenda Ronaldo ambaye aliwahi kuichezea Spoting Lisbon akashuka zaidi kwenye orodha ya mapato ikiwa timu yake ya zamani ya Manchester United itamsajili Gjiwi wa Chile anayeichezea klabu ya Arsenal Alexis Sanchez.
Tuma neno ‘NEWS’ kwa 40227 ili kupata habari muhimu pindi zinapochipuka
Habari Nyingine: Muimbaji wa Tanzania - Ray C - asema angependa kuolewa na Rais Uhuru, atoa sababu
Lionel Messi wa klabu ya Barcelona anaongoza kwenye orodha hiyo baada ya kutia saini kandarasi mpya ya paundi 780,000 kila wiki katika klabu ya Barcelona na kumshinda Cristiano.
Habari Nyingine: Pasta ahamishwa kwa nguvu Baba Dogo kwa kuwakataza waumini kula nyama!
Mshambulizi wa zamani wa Manchester United anayeichezea Manchester City Carlos Teves ni wa pili kwa kipato cha paundi 650,000 kila wiki, licha ya kuwa na msimu mbaya zaidi kwenye taaluma yake alipokosa kucheza mechi kadhaa na kuongeza uzani wake.
Mchezaji mahiri wa PSG Neymar huenda alikubali kushuka hadhi alipoondoka La Liga na kwenda kwenye Ligue 1 lakini aliimarisha mapato yake kuwa paundi 609,000 kila wiki, akiwa katika nafasi ya tatu.
Habari Nyingine: Kimenuka! Diamond Platinumz aonyesha ‘udume’ wake kwa kumzaba kofi mke wake
Aliyekuwa mchezaji wa klabu ya Chelsea Oscar dos Santos yuko kwenye nafasi ya nne baada ya uhamisho wake kwenye ligi ya Uchina ambapo anapata paundi 400,000 kila wiki. Ezequiel Lavezzi anayeichezea klabu ya Uchina ya Hebeli China Fortune anamaliza orodha ya tano bora kimapato kwa mshahara wa paundi 388,000 kila wiki.
Cristiano Ronaldo yuko kwenye nafasi ya sita akipata paundi 355,000 kila wiki kutoka Real Madrid.
Habari Nyingine: Je wanaume wanahitaji nini katika uhusiano? Wakenya watoa maoni yao
Ilidaiwa kuwa Ronaldo alikuwa ameitisha nyongeza ya mshahara ambayo huenda ikaimarisha mapato yake kuwa sawa na ile ya Lionel Messi wa Barcelona.
Read ENGLISH VERSION
Una maoni? Una taarifa ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri: mwangi.muraguri@tuko.co.ke
Chanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2Bvzmeinmdia4B4go9mpJ6ro556osPAqKWgp6qWeritzZqqqKORYoJusNSnoJqmmWLEorrAqKOiqKeWerutyJ2gZpuinsC1tcCnpmaqn6OurbDOZpikoaOdwqytjKGYnaCZYriqssSdn5pmmKm6rQ%3D%3D